Naibu Waziri Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Mhe. Lulu Msham Abdalla akiwa na mazungumzo na Mkurugenzi Idara ya Misitu na Maliasili Zisizorejesheka Nd. Soud Mohamed Juma kwenye ofisi za Idara ya Misitu  Maruhubi kabla ya kukabidhi vitendea kazi kwa wadau wa Misitu (mwenye nasari binafsi).

Jumla ya miche milioni mbili na laki tano (2,500,000) inatarajiwa kupandwa katika msimu wa kilimo mwaka 2017/18 katika  Idara ya misitu na maliasili zisizorejesheka .
Akikabidhi vitendea kazi  kwa vitalu vya uzalishaji miche binafsi kwa vikundi kumi na saba kutoka wilaya Kaskazin B,  Maharibi A na B   na Naibu waziri Wizara Kilimo,Maliasili, Mifugo na Uvuvi Mhe Lulu Msham Abdalla huko Maruhubi katika ofisi za Idara ya misitu na maliasili Zisizorejesheka.
Amesema Wizara  kupitia Idara ya Misitu INA  lengo la kuhakikisha  miche  inapatikana kwa wananchi wote ili kuhifadhi na kulinda mali  asili, mazingira na mali zisizorejesheka.

  

Mhe. Lulu akikabidhi vitendea kazi kwa mdau wa misitu (mwenye nasari binafsi).
Mhe, Lulu amesema kuwa mpango huo utasaidia kuweka hewa safi  na afya kwa jamii ili kukuza uchumi katika nchi, pia aliwataka kuvitunza na kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuweza kufikia malengo
Nao wazalishaji wa miche ya matunda na misitu wameiomba  Idara ya misitu kuendeleza utaratibu wa utoaji wa vifaa na kupatiwa elimu zaidi ya uzalishaji wa miche kwani wanapata changamoto nyingi kwenye kazi ya hiyo.
Jumla ya shilingi milioni nne (4,000,000) zimetumika kwa ajili ya  kununulia vifaa  kwa wazalishaji wa  miche kwa  msimu wa kilimo 2017/18  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii